Naibu Waziri Nderiananga atoa wito kwa ASA, aipongeza uzalishaji mbegu

MOROGORO-Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga ameupongeza uongozi wa Wakala wa Taifa wa Uzalishaji na Uendelezaji wa Mbegu za Kilimo (ASA) kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuzalisha na uendelezaji wa mbegu nchini.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. Ummy Nderiananga akionesha mimea iliyo katika maabara maalumu alipotembela ofisi za Wakala wa Taifa wa Uzalishaji na Uendelezaji wa mbegu za kilimo (ASA) mkaoni Morogoro.Ni ziara ya kukagua utekelezaji wa Programu wa Kuendeleza Kilimo na Uvuvi AFDP inayoratibiwa na Ofisi yake.

Pia,amewasihi kuendelea kuzingatia ubora na weledi katika majukumu ya kuzalisha mbegu bora hizo ili kuendelea kuwa na uhakika wa chakula cha kutosha nchini.

Ametoa pongezi hizo wakati wa ziara yake ya kikazi kufuatili shughuli za utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo na Uvuvi ya AFDP ambayo inaratibiwa na ofisi yake na kutekeleza katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo Morogoro.
Afisa Kilimo ASA Bw. Josephat Masanja akimuonesha mitambo ya kuchakata mbegu katika maabara maalum Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga alipofanya ziara yake katika ofisi za ASA mkoani Morogoro alipokagua utekelezaji wa Programu wa Kuendeleza Kilimo na Uvuvi AFDP inayoratibiwa na Ofisi yake.

Akiwa katika ziara hiyo alitembelea Kituo cha Kuendeleza Ukuzaji Viumbe Maji Kingolwira, Wakala wa Taifa wa Uzalishaji na Uendelezaji wa mbegu za kilimo (ASA) Pamoja na Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) zilizopo mkoani Morogoro.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mhe. Ummy Nderiananga akizungumza na Mkurugenzi wa Uzalishaji ASA Dkt. Justin Ringo alipotembelea na kukagua utekelezaji wa Programu wa Kuendeleza Kilimo na Uvuvi AFDP inayoratibiwa na Ofisi yake mkoani Morogoro.

Mhe.Ummy amesema upo umuhimu wa kuendelea kuunga mkono Programu ya kuendeleza sekta ya Kilimo na Uvuvi nchini kwa kuzingatia inaongeza tija hasa katika kuhakikisha kunakuwa na mbegu bora nchini.
“Ofisi ya Waziri Mkuu tunaendelea kufanya uratibu na kutathmini ya programu hii ambayo ni ya miaka sita hivyo endeleeni kufanya kazi vizuri, kwa weledi huku mkiunga jitihada za Mhe Rais za kuona Tanzania inakuwa ghala kubwa la chakula, Serikali haita waacha nyumba, inaendelea kuunga mkono jitihada hizi,”alisema Mhe.Nderiananga.

Aidha aliwataka kuendelea kuzingatia ubora na viwango katika utekelezaji wa majukumu ya uzalishaji wa mbegu bora na zinazoendana na mahitaji halisi.
Mkurugenzi wa Uzalishaji kutoka Wakala wa Taifa wa Uzalishaji na Uendelezaji wa mbegu za kilimo (ASA) Dkt. Justin Ringo akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga kuhusu shughuli zinazofanywa katika mashine za kuchakata mbegu, wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Programu wa Kuendeleza Kilimo na Uvuvi AFDP inayoratibiwa na Ofisi yake Mkoani Morogoro.

“Eneo la mbegu ni muhimu sana, bila kuwa na mbegu nzuri hatuwezi kuwa na matokeo ya chakula kizuri, hivyo ninawapongeza mnafanya kazi nzuri endeleeni maana tunategemea sana sekta yetu ya kilimo ili kuendelea kuwa na uhakika wa chakula nchini,”alisisitiza.

Kwa upande wake Mchumi Mwandamizi kutoka wa Wakala wa Taifa wa Uzalishaji na Uendelezaji wa Mbegu za Kilimo (ASA), Bw. Edmund Kayombo akizungumza kuhusu wakala hiyo amesema, umeendelea kutoka huduma za kuongeza uzalishjaji na usambazanji mbegu bora.
Mkurugenzi wa Uzalishaji kutoka Wakala wa Taifa wa Uzalishaji na Uendelezaji wa mbegu za kilimo (ASA) Dkt. Justin Ringo akimuonesha Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga moja ya mbegu aina ya maharage zilizoandaliwa na Wakala huo, wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Programu wa Kuendeleza Kilimo na Uvuvi AFDP inayoratibiwa na Ofisi yake Mkoani Morogoro.

Sambamba na kuhamasisha sekta binafsi kushiriki katika uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora, kuhamasisha wakulima kutumia mbegu bora na kushirikiana na kituo cha utafiti ili kuhakikisha mbegu mpya zinazaliwashwa na kusambazwa kwa wakulima.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga Pamoja na timu aliyoongozana nayo akiwa katika picha ya Pamoja na watumishi wa Wakala wa Taifa wa Uzalishaji na Uendelezaji wa mbegu za kilimo (ASA) mara baada ya ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo na Uvuvi - AFDP inayoratibiwa na Ofisi yake.(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU).

“Wakala wa Mbegu za kilimo una jumla ya mashamba 14 ikiwemo mashamba ya kilimo yaliyopo Nzenga, Msungula (Kasulu), Chalinze, Nane nane - Morogoro, Tanganyika, Dabaga kilosa, Arusha (Tengelu), Namtumbo (Songera), Njombe, ambayo yanajumla ya ukubwa wa hekta 16,909,”amesema Kayombo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news