Subira yavuta heri, vyakula mbioni kushuka bei Zanzibar

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema, Serikali imeanza kuchukua hatua kukabiliana na upandaji wa bei za vyakula hasa mchele na sukari nchini.

Mheshimiwa Rais Dkt.Mwinyi ameyasema hayo Septemba 25, 2023 Ikulu jijini Zanzibar wakati akizungumza na wafanyabiashara wanaoagiza vyakula nje ya nchi na watendaji wa Serikali.

Amesema, matarajio ya Serikali ni kurudisha bei za awali kwa bidhaa zilizopo madukani, pia ameagiza Serikali kutoa fedha zake za kigeni na kuwapa kipaumbele wafanyabiashara hususani waagizaji vyakula nje ya nchi, hivyo amewataka wafanyabiashara hao kushirikiana kuagiza bidhaa hizo kwa pamoja.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Rais Dkt.Mwinyi amegusia suala la mizigo kushukia Bandari ya Mkoani ili kupunguza gharama za bidhaa Pemba.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news