Akizungumzia huduma maalum za ushauri wa Kitaalamu, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji huyo amesema, benki yao imetoa ushauri wa kitaalamu katika miradi ya kimkakati ikiwemo ATCL na TTCL. Sambamba na utengenezaji wa mpango wa biashara wa muda wa kati.
Amesema, mradi wa TPDC ni wa utafutaji wa gesi (gas exploration), katika Bahari ya Hindi kupitia Kampuni ya M&P, ambapo waliweza kuwahudumia kupitia mpango huo, wakati kwa TANESCO ni kupitia mradi wa utanuzi wa huduma za umeme mijini.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji huyo ameongeza kwamba, kupitia mpango wa kibiashara na fedha, walitoa ushauri wa kitaalamu wa mradi wa DART. Pia, kwa TPA waliangazia katika mpango wa kibiashara na fedha kwa ajili ya mradi wa Bandari ya Bagamoyo na ushauri wa kitaalamu katika uendeshaji miradi ya Bandari ya Bagamoyo.
Vile vile, TRL ni kupitia mpango wa kibiashara na fedha, ushauri wa kitaalamu wa mradi wa TRL, Mradi wa Bomba la Mafuta (EACOP)- Hoima (Uganda)-Tanga (Tanzania) na Mfuko wa Msaada wa Kiufundi, huku benki hiyo ikitenga fungu maalum kwa ajili ya kusaidia taasisi na mashirika kuandaa miradi inayokidhi vigezo vya uwekezaji na mikopo.
Miradi mingine iliyofaidika na mfuko huu ni Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi cha Mbezi Louis (Magufuli Bus Terminal), kupitia Jiji la Dar es Salaam (DDC), Mradi wa Soko la Kisasa la Kisutu kupitia Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, mradi wa Kiwanda cha Kuchakata zabibu kilichopo Chinangali katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma.