Ukusanyaji mapato ya Serikali unaridhisha-MPC

NA GODFREY NNKO

KAMATI ya Sera ya Fedha (MPC) ya Benki Kuu imebaini kuwa,ukusanyaji wa mapato ya Serikali kwa Tanzania Bara ulikuwa wa kuridhisha ambapo makusanyo yalifikia asilimia 96.2 ya lengo katika robo ya kwanza ya mwaka 2023/24.

Hayo yamebainishwa kupitia taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye ni Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Tutuba baada ya kamati kufanya mkutano wake wa 228 tarehe 27 Oktoba 2023.

Lengo la mkutano huo ulikuwa ni kutathmini utekelezaji wa Sera ya Fedha na mwenendo na mwelekeo wa uchumi.

Kwa upande wa Zanzibar, ukusanyaji wa mapato ulivuka lengo kwa asilimia 1.7. Matumizi ya Serikali yameendelea kufanyika kulingana na mapato.

Vile vile. Gavana Tutuba amefafanua kuwa. nakisi ya urari wa biashara, huduma na uhamisho mali nje ya nchi imeendelea kuwa kubwa kutokana na kupanda kwa bei za bidhaa katika Soko la Dunia.

"Hata hivyo nakisi hii ilipungua kufikia dola milioni 3,652.6 kwa mwaka unaoishia Septemba 2023, kutoka dola milioni 4,728.1 kwa mwaka ulioishia Septemba 2022, kutokana na ongezeko la mapato yanayotokana na shughuli za utalii.

"Nakisi hii inatarajiwa kupungua zaidi kutokana na kuendelea kuongezeka kwa mapato yatokanayo na shughuli za utalii, mauzo ya dhahabu na mazao ya biashara nje ya nchi."

Gavana Tutuba amebainisha kuwa, kwa upande wa Zanzibar nakisi ya urari wa biashara,huduma na uhamisho mali nje ya nchi ilifikia dola za Marekani milioni 417.1 ukilinganisha na dola za marekani milioni 344.4, kutokana na ongezeko la gharama za uagizaji wa bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi.

Wakati huo huo, MPC imebainisha kuwa, utekelezaji wa sera ya fedha, pamoja na sera thabiti za kibajeti, na kimfumo, zimesaidia kukabiliana na shinikizo la mfumuko wa bei, kuchangia ukuaji wa shughuli za kiuchumi na uhimilivu wa sekta ya fedha nchini licha ya mtikisiko wa kiuchumi duniani.

Aidha, utekelezaji wa sera ya fedha pia umesaidia kupunguza shinikizo linalotokana na ongezeko la mahitaji ya fedha za kigeni nchini.

Kamati pia, ilitathmini mwenendo wa uchumi wa dunia kwa mwaka 2023 na kubaini kuwa, uchumi wa dunia bado haujaimarika licha ya ukuaji wa juu ya matarajio uliofikiwa katika kipindi cha nusu ya kwanza ya mwaka. 

Mwenendo huu unatokana na kubanwa kwa sera ya fedha katika nchi nyingi duniani, migogoro ya kisiasa na ongezeko la bei za mafuta.

Wakati huo huo, MPC imebainisha kuwa, utekelezaji wa sera ya fedha, pamoja na sera thabiti za kibajeti, na kimfumo, zimesaidia kukabiliana na shinikizo la mfumuko wa bei, kuchangia ukuaji wa shughuli za kiuchumi na uhimilivu wa sekta ya fedha nchini licha ya mtikisiko wa kiuchumi duniani.

Aidha, utekelezaji wa sera ya fedha pia umesaidia kupunguza shinikizo linalotokana na ongezeko la mahitaji ya fedha za kigeni nchini.

Kamati pia, ilitathmini mwenendo wa uchumi wa dunia kwa mwaka 2023 na kubaini kuwa, uchumi wa dunia bado haujaimarika licha ya ukuaji wa juu ya matarajio uliofikiwa katika kipindi cha nusu ya kwanza ya mwaka. 

Mwenendo huu unatokana na kubanwa kwa sera ya fedha katika nchi nyingi duniani, migogoro ya kisiasa na ongezeko la bei za mafuta.
 
Mbali na hayo, kwa kuzingatia mwenendo wa uchumi wa dunia na wa hapa nchini, Kamati ya Sera ya Fedha iliamua kuendelea na utekelezaji wa sera ya fedha inayolenga kupunguza kasi ya ongezeko la ukwasi katika uchumi.

Pia, amebainisha kuwa, Sera ya fedha itaendelea kutekelezwa sambamba na sera za kibajeti na kimuundo ili kufikia malengo ya kiuchumi.

Aidha,amesema utekelezaji wa Sera ya Fedha unalenga kuhakikisha malengo yaliyoainishwa kwenye programu ya Extended Credit Facility (ECF) kwa robo inayoishia Desemba 2023 yanafikiwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news