Wauza dawa za kulevya Tanga kukiona

TANGA-Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga, ACP Almachius Mchunguzi amesema,kwa sasa jeshi hilo linaendelea kufanya msako kuhusu uingizwaji wa dawa za kulevya na tayari baadhi ya watumiaji wameshatiwa mbaroni.


ACP Mchunguzi amesema,wanaohitajika zaidi ni wale ambao wanauza kwani bila kuwakamata wao biashara hiyo haitakoma. Ameyasema hayo wakati wa matembezi maalumu ya kulinda amani ya jeshi hilo mkoani Tanga.

"Mpango wa kudhibiti dawa za kulevya tunaendelea nao na tayari wapo watu wameshakamatwa, mkoa wetu ni njia ya kupitishia, lakini tunapokamata watumiaji tu haitoshi, inatupasa tupambane na wale wakubwa ambao ni wauzaji ili tuweze kukomesha vitendo hivi.

"Baadhi yao tuna majina yao, sasa niwaambie tu wajisalimishe hata kwa kujitetea, lakini kwa watakaendelea msako wetu utakapompitia kitakachotokea ni maumivu kwake kwa kuwa amekataa kutii sheria bila shuruti,"amesema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news