Mkurugenzi wa NHC aueleza uongozi wa Kiwanda cha Marumaru cha Keda mikakati ya shirika

PWANI-Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Hamad Abdallah amefanya mazungumzo na Uongozi wa Kiwanda cha Marumaru cha Keda na kutembelea maeneo mbalimbali ya kiwanda hicho kilichopo Chalinze mkoani Pwani.
Katika mazungumzo hayo,Mkurugenzi Mkuu aliuambia Uongozi wa kiwanda hicho kuwa NHC inatembelea viwanda mbalimbali kuona uwezo, gharama na muda utakaotumika kuzalisha vifaa vya ujenzi vitakavyosaidia NHC kujenga nyumba za gharama nafuu kwa Watanzania.
Tangu aingie NHC, Hamad amehimiza kupunguza gharama ya ujenzi wa nyumba kwa kununua vifaa vya ujenzi moja kwa moja kutoka viwandani ambako bei na ubora wa vifaa hivyo unakubalika katika kuwezesha ujenzi wa nyumba bora na kwa gharama nafuu.
Uongozi wa kiwanda hicho umeonyesha nia ya kufanya kazi na NHC katika kuchangia ujenzi wa nyumba bora na nafuu nchini Tanzania. Kiwanda hicho kinazalisha mita za mraba 50,000 za marumaru kwa siku na kinafanya kazi siku 7 za wiki kwa saa 24.
Ziara hii ni muendelezo wa ziara mbalimbali zinazofanywa na NHC katika viwanda vya kutengeneza vifaa vya ujenzi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news