RC Chalamila, Dkt.Yonazi washiriki IFM Alumni Marathon

DAR ES SALAAM-Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila leo Novemba 19,2023 ameshiriki IFM Alumni Marathon ambayo imeandaliwa na Watumishi na Wanafunzi waliosoma katika chuo hicho cha Usimamizi wa fedha ambao kwa sasa wanafanya kazi maeneo mbalimbali hapa nchini.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila (kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu Ofisi ya Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi (kushoto) wakati wa IFM Alumn Marathon ambayo imeandaliwa na Watumishi na Wanafunzi waliosoma katika chuo hicho cha Usimamizi wa fedha ambao kwa sasa wanafanya kazi maeneo mbalimbali hapa nchini, hafla hiyo ilifanyika The Grounds, Oysterbay Jijini Dar es Salaam tarehe 19 Novemba, 2023.

Akiongea mara baada ya kukimbia umbali wa kilometa 5 Mhe. Chalamila amekipongeza chuo hicho kwa kubuni matembezi hayo ambayo mapato yanayopatikana yanatumika katika maendeleo ya Chuo.
Katibu Mkuu Ofisi ya Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi akigawa vyeti kwa washariki wa IFM Alumn Marathon ambayo imeandaliwa na Watumishi na Wanafunzi waliosoma katika chuo hicho cha Usimamizi wa fedha ambao kwa sasa wanafanya kazi maeneo mbalimbali hapa nchini.

"Jambo linalofanywa na IFM ni la Kizalendo nitoe rai kwa vyuo vingine kuiga mfano huo wa kibunifu ambao una masilahi mapana sio tu kwa chuo bali hata Taifa kwa ujumla,"amesema Mhe. Chalamila.
Katibu Mkuu Ofisi ya Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi akigawa vyeti kwa washariki wa IFM Alumn Marathon ambayo imeandaliwa na Watumishi na Wanafunzi waliosoma katika chuo hicho cha Usimamizi wa fedha ambao kwa sasa wanafanya kazi maeneo mbalimbali hapa nchini.

Aidha, amewataka kufanya maboresho katika matembezi hayo kwa kushirikisha makundi mengi zaidi kwa mfano kundi la jogging ili kuweza kusambaza ujumbe ufike mbali zaidi, vilevile ametoa Salamu za Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambapo amesema Rais anawasalimu na anafurahishwa na kitendo hiki cha kutambua umuhimu wa mazoezi katika Afya ya Binadamu.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi ambaye pia ni mwenyekiti wa umoja huo alishiriki mbio hizo kwa umbali wa kilomita 5.
Katibu Mkuu Ofisi ya Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa IFM Alumn Marathon ambayo imeandaliwa na Watumishi na Wanafunzi waliosoma katika chuo hicho cha Usimamizi wa fedha ambao kwa sasa wanafanya kazi maeneo mbalimbali hapa nchini.

Dkt. Yonazi amesema kuwa marathon hiyo imehusisha watu ambao walisoma IFM, na marafiki ili kuleta umoja wa wana IFM na kuongezea kuwa mbio hizo huchangia maendeleo ya Chuo na Taifa, pia amewashukuru wadhamini wote waliojitoa kwa hali na mali kuwezesha kufanyika kwa mbio hizo.
Katibu Mkuu Ofisi ya Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa IFM Alumn Marathon ambayo imeandaliwa na Watumishi na Wanafunzi waliosoma katika chuo hicho cha Usimamizi wa fedha ambao kwa sasa wanafanya kazi maeneo mbalimbali hapa nchini.

Naye Mkamu Mkuu wa chuo hicho Dkt. Mnzava amemshukuru Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa kwa kuungana nao katika mbio hizo ambapo amesema ni tukio la kihistoria na ni mara ya kwanza toka chuo kianze mwaka 1972, amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kuendeleza mbio hizo, kwa kuhamasisha makundi mbalimbali kushiriki kwa kuwa mazoezi ni Afya kama kauli mbiu inavyosema "Badili Mwenendo Wako wa Maisha kwa Afya Bora."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news