Benki Kuu yaendelea kuyafikia makundi mbalimbali utambuzi wa alama za noti, utunzaji fedha

MOROGORO-Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa mafunzo maalumu ya namna bora ya utambuzi wa alama za noti kwa makundi maalumu mkoani Morogoro.
Makundi hayo yanajumuisha watu wenye ulemavu wa viungo, ngozi, uoni hafifu ,viziwi na watu wanaoishi katika mazingira magumu.
Aidha, BoT imetoa mafunzo ya namna sahihi ya kutunza fedha kwa ajili ya matumizi yao huku ikiwataka kuwa mabalozi wazuri wa kufundisha wenzao namna ya kutunza fedha.
BoT inatoa mafunzo hayo ya siku tatu kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la SEED (Social and Economic Empowerment of the Disadvantaged) linalojishughulisha na kuwawezesha watu wenye ulemavu na wanaoishi katika mazingira magumu.
Fahamu Jukumu la BoT

Jukumu la msingi la Benki Kuu ya Tanzania ni kuandaa na kutekeleza sera ya fedha inayolenga kudhibiti mfumuko wa bei na kujenga mfumo wa fedha ulio imara na unaofaa kwa ukuaji endelevu wa uchumi wa taifa.

Majukumu mengine ya Benki Kuu ya Tanzania
  • Kutoa sarafu ya nchi ambayo ni Shilingi ya Tanzania
  • Kusimamia na kudhibiti mabenki na taasisi za fedha
  • Kusimamia na kudhibiti mifumo ya malipo nchini.
  • Kuhifadhi akiba ya nchi ikiwemo fedha za kigeni
  • Benki ya Serikali
  • Benki ya Mabenki; na
  • Kutoa ushauri juu ya masuala ya uchumi na fedha kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news