Chatanda azindua Kamati ya Mapambano dhidi ya Ukatili wa Wanawake na Watoto

DAR ES SALAAM-Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Chatanda leo amezindua Kamati ya Mapambano dhidi ya Ukatili wa Wanawake na Watoto.
Akizindua kamati hiyo katika Viwanja vya Mnazi Mmmoja jijini Dar es Salaam leo, Mama Chatanda amesema uundwaji wa kamati hii ni kutokana na Maelekezo ya Mh Rais Dr. Samia Suluhu Hassan katika hotuba yake kwenye mkutano wa UWT pale Dodoma.
"Majukumu ya kamati hii ni kuweka Mikakati ya kushughulikia na kutokomeza vitendo vya ukakatili uzalilishaji kwa wanawake na watoto kama vile ubakaji na ulawiti,"amesema Chatanda.
Pia ametoa maelekezo kwa kuhakikisha mikoa inaunda kamati ya Mapambano dhidi ya ukatili kwenye ngapi zote za Uongozi na kupanga Ratiba ya Viongozi wa UWT kutembelea madawati ya Jinsia na kuhakikisha taarifa ya kesiza ukatili na hatua zilizofikia zinawasilishwa makao makuu.
Amesema,pia kamati hiyo itaweza kuishauri kamati ya msaada wa Kisheria kesi ambazo zinahitaji msaada wa kisheria kutoka UWT.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news