Simba SC yatoshana nguvu na Jwaneng Galaxy FC

FRANCIS TOWN-Klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam nchini Tanzania imeshindwa kuonesha umahiri wake ugenini katika Michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika.
Ni baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana dhidi ya wenyeji, Jwaneng Galaxy FC ya nchini Botswana.

Mtanange huo wa Kundi B umepigwa leo Desemba 2, 2023 katika Dimba la Francistown lililopo Francistown nchini Botswana.

Simba SC walishindwa kutumia nafasi walizozipata kutoka kwa wenyeji hao huku wakiwa na Kocha wao mpya Abdelhak Benchikha licha ya mara nyingi kuonekana kuutawala mtanange huo.

Aidha, kwa matokeo hayo Simba wamefikisha alama mbili baada ya kutoka sare ya kufungana bao 1-1 na ASEC Mimosas ya Ivory Coast huku Jwaneg Galaxy wanafikisha alama nne.

Watswana hao wiki iliyopita walianza kwa ushindi wa ugenini wa 1-0 dhidi ya Wydad Athletic jijini Marrakech nchini Morocco.

Hata hivyo, wawakilishi hao wa Tanzania katika michuano ya Kimataifa watashuka tena dimbani Desemba 9, mwaka huu kucheza na wenyeji Wydad Casablanca nchini Morocco.

Wakati huo huo,Jwaneng ya Botswana watakuwa wenyeji dhidi ya ASEC Mimosas siku hiyo katika Dimba la Francistown nchini Botswana.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news