Ujenzi maabara shule za Musoma Vijijini

MARA-Jimbo la Musoma Vijijini limeamua kutatua tatizo sugu la ukosefu wa maabara za masomo ya sayansi kwenye sekondari zake za kata.

Lengo kuu:
Kila Sekondari ya Kata ipate maabara nzuri na za kisasa za masomo matatu ya sayansi - physics, chemistry & biology labs.

Wachangiaji wakuu wa mradi huu ni:
1. Wanavijiji
2. Serikali Kuu
3. Mbunge wa Jimbo
4. Mfuko wa Jimbo
5. Baadhi ya wazaliwa wa Musoma Vijijini

Halmashauri yetu (Musoma DC) inaendelea kushauriwa nayo ianze kuchangia mradi huu kwa kutumia mapato yake ya ndani!

Takwimu za maabara tulizonazo:

(A) Sekondari zenye maabara tatu (3):
1. Bugwema 2. Kiriba
3. Ifulifu 4. Mugango
5. Bwai (zinakamilishwa Jan 2024)

(B) Sekondari zenye maabara mbili (2):
6. Bulinga 7. Kigera
8. Nyakatende 9. Makojo
10. Nyambono 11. Nyegina
11. Rusoli 13. Suguti

(C) Sekondari zenye maabara moja (1):
14. Bukima 15. Dan Mapigano (Bugoji)
16. Etaro 17. Kasoma
18. Mabuimerafuru

(D) Sekondari zizokuwa na maabara hata moja
19. Nyegina 20. Busambara
21. Mtiro 22. Murangi
23. Nyanja 24. Seka
25. Tegeruka

Sekondari za binafsi zimejenga maabara zake
26. Bwasi (Kanisa la Wasabato/SDA)
27. Nyegina (Kanisa Katoliki/RC)

Karibuni tuendelee kuchangia ujenzi wa maabara za masomo ya sayansi kwenye sekondari zetu za kata za Musoma Vijijini

Tafadhali sana usisahau harambee ya ujenzi wa maabara za Etaro Sekondari utakaofanyika Ijumaa, 15.12.2023 (tangazo la harambee linatolewa leo)

Sayansi ni kila kitu
&
*Kila kitu ni Sayansi

Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news