China, Zanzibar zasaini MoU

ZANZIBAR-Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar imetiliana saini Hati ya Mashirikiano na Wizara ya Maliasili na Bahari ya Jamhuri ya Watu wa China.
Makubakiano hayo yamesainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Aboud Hussein Jumbe na Naibu Waziri wa Wizara ya Maliasili na Bahari ya Jamhuri ya Watu wa China,Mhe. Dkt. Sun Shuxien.

Sekta zitakazohusika na makubakiana hayo ni pamoja na Sekta ya Uchumi wa Buluu ikiwemo Sayansi na Teknolojia ya Baharini, Uchunguzi wa Mazingira ya Bahari, utabiri wa ufuatiliaji na tathmini ya kujikinga na maafa ya majanga baharini.

Pia makubakiano hayo yatahusisha Utafiti wa Baharini, kujengea uwezo, uwekezaji, uhifadhi wa viumbe hai wa baharini na ulinzi wa mfumo wa ikolojia wa baharini, pamoja na maeneo mengine ya Uchumi wa Buluu.

Mbali na hayo Jamhuri ya Watu wa China pia itatoa fursa za ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wa Kizanzibari katika fani za Uchumi wa Buluu na Usimamizi wa bahari.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news