Kamati ya Bunge yaipa kongole Wizara ya Ardhi uboreshaji mfumo

NA MUNIR SHEMWETA
WANMM

KAMATI ya Kudumu ya Bunge Ardhi Maliasili na Utalii imeipongeza Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kufanya kazi kubwa na nzuri ya maboresho ya Mfumo Unganishi wa Usimamizi wa Sekta ya Ardhi inayofanywa na timu ya wataalamu mkoani Arusha.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mhe. Timotheo Mzava akizungumza wakati kamati yake ilipotembelea kazi ya uboreshaji Mfumo Unganishi wa Usimamizi wa Sekta ya Ardhi inayofanywa na timu ya wataalamu mkoani Arusha tarehe 8 Januari 2023.

Akizungumza mara baada ya hitimisho la wasilisho la kazi ya uboreshaji mfumo huo, Mwenyekiti wa kamati, Mhe. Timotheo Mzava ameipongeza Wizara ya Ardhi kwa kazi kubwa na nzuri na kueleza kuwa, kazi hiyo inakwenda kuacha alama kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan katika kipindi chake cha uongozi kwa kuiacha sekta ya ardhi katika mifumo bora.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Geophrey Pinda akizungumza wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii ilipokwenda jijini Arusha kukagua kazi ya Uboreshaji Mfumo Unganishi wa Usimamizi wa Sekta ya Ardhi tarehe 8 Januari 2024.

"Nichukue fursa hii kumpongeza Mhe.Rais kwa kazi hii nzuri, kama kamati wameridhishwa na kazi na hongereni sana na mfumo huu uende ukawe bora na kutoa huduma kwa watanzania," alisema Mhe Mzava.

Baadhi ya wabunge wamesema, mfumo huo siyo tu utarahisisha na kuharakisha huduma za sekta ya ardhi bali utajibu maswali mengi yakiwemo ya kijamii.
Mbunge wa Viti Maalum CCM, Lucy Mayenge akichangia hoja wakati Kamati ya Bunge Ardhi Maliasili na Utalii ilipotembelea na kupata taarifa ya kazi ya uboreshaji Mfumo Unganishi wa Usimamizi wa Sekta ya Ardhi inayofanywa na timu ya wataalamu mkoani Arusha tarehe 8 Januari 2023.

"Niipongeze wizara ya ardhi kwa kufanyia kazi mfumo utakaojibu maswali mengi ya kijamii na ningetamani mfumo huu ungejibu maswali na changamoto za kiuchumi," alisema Mhe. Lucy Mayenga mbunge wa viti maalum.

Mbunge wa Makete mkoani Njombe, Festo Sanga aliipongeza wizara kwa kuboresha mfumo na kueleza kuwa uboreshaji huo umechelewa ingawa uko katika hatua nzuri.
Mbunge Festo Sanga akichangia hoja wakati Kamati ya Bunge Ardhi Maliasili na Utalii ilipotembelea kazi na kupata taarifa ya uboreshaji Mfumo Unganishi wa Usimamizi wa Sekta ya Ardhi inayofanywa na timu ya wataalamu mkoani Arusha tarehe 8 Januari 2023.

Hata hivyo, mbunge huyo wa Makete alitaka kufahamu utayari wa Wizara ya Ardhi katika kutumia mfumo hususan kwenye eneo la usalama wa mifumo.

Aidha, Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini,Emanuel Adamson mbali na kuipongeza wizara kwa kuboresha mfumo alitaka kufahamu uimara wa utekelezaji mfumo huo kwa kuwa kumekuwa na mifumo mingi lakini wakati wa utekekezaji kumekuwa na changamoto ikiwemo kuekezwa mtandao uko chini.
Baadhi ya wataalamu wanaofanya kazi ya kufanya Maboresho Mfumo Unganishi wa Usimamizi wa Sekta ya Ardhi. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI).

Mfumo huo unganishi wa usimamizi wa sekta ya ardhi unatarajiwa kuanza katika mikoa mitano ya Arusha, Dodoma, Mwanza, Mbeya na Tanga na utarahisisha na kuharakisha upatikanaji huduma za sekta ya ardhi kwa kuwa wananchi watakuwa wakipata huduma kwa njia ya mtandao.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news