EAC:Hatujazindua noti mpya ya pamoja (SHEAFRA)

ARUSHA-Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imewataka wadau wake wote kupuuza taarifa iliyosambaa mitandaoni ikidai kuwa imetambulisha noti mpya ya pamoja itakayotumika katika nchi wanachama iitwayo SHEAFRA.

"Sekretarieti ya EAC inapenda kuwafahamisha wadau wetu wote kwamba safari ya nchi wanachama katika kutumia sarafu moja bado kazi inaendelea.

"Tafadhali puuzeni uvumi wowote unaosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kuzindua noti mpya za eneo hili.
EAC ni jumuiya ya kiserikali inayoundwa na nchi saba za Afrika Mashariki ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Burundi, Kenya, Rwanda, Sudan Kusini, Uganda na Tanzania.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news