Tanzania, Burundi zasaini MoU kwenye Sekta ya Madini

BUJUMBURA-Mawaziri wa Sekta ya Madini wa Burundi, Mheshimiwa Mhandisi Ibrahim Uwizeye na Tanzania Mheshimiwa Anthony Mavunde leo wamesaini hati ya makubaliano ya kushirikiana kwenye sekta ya madini ili kukuza mchango wa sekta hii katika uchumi wa nchi mbili hizi.
Hafla ya kusaini makubaliano hayo imefanyika leo jijini Bujumbura,Burundi na kuhudhuriwa na watalaamu wa nchi zote mbili.

Maeneo ya Ushirikiano yanajumuisha;

- Ujenzi wa Viwanda vya Uchenjuaji na Usafishaji wa Madini.

- ⁠Kubadilishana Uzoefu na utaalamu katika utafiti wa kina wa madini.

- ⁠Kuongeza thamani ya madini kwa kuzalisha bidhaa zitokanazo na madini.

- ⁠Kujenga uwezo wa kitaasisi na wataalamu wa pande zote mbili.

- ⁠Kusimamia sheria na taratibu za biashara ya madini inayohusisha pande zote mbili.
Akitoa maelezo ya awali Waziri wa Maji,Nishati na Madini wa Jamhuri ya Burundi,Mheshimiwa Mhandisi Ibrahim Uwizeye amesema nchi ya Burundi na Tanzania zimekuwa na urafiki wa muda mrefu na mahusiano mazuri.

Hivyo,ni muhimu kutumia fursa hii kushirikiana kwenye sekta ya madini ili sekta hii itoe mchango unaostahili katika kukuza maendeleo ya uchumi wa Burundi na Tanzania chini ya uongozi imara wa marais Mheshimiwa Evariste Ndayishimiye (Burundi) na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan (Tanzania).
Akizungumza katika hafla hiyo,Waziri wa Madini wa Tanzania,Mheshimiwa Anthony Mavunde amesema,Tanzania ipo tayari kushirikiana na Burundi katika kuiimairisha na kuiboresha sekta ya madini ya nchi hizi mbili kwa kusimamia utekelezaji wa makubaliano ya ushirikiano yaliyofikiwa na kutumia fursa hii kuwaalika wachimbaji wa nickel,cobalt na copper.
Pia, kutumia huduma ya Kiwanda cha Usafishaji madini ambacho kitajengwa katika eneo la ulipokuwa Mgodi wa Buzwagi wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news