Tanzania,Ghana zabadilishana uzoefu kuhusu Hakimiliki

ACCRA-Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma amekutana na kufanya mazungumzo na Ofisi ya Hakimiliki ya nchini Ghana ikiongozwa na William Bonsu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na baadhi ya wataalamu wa Hakimiliki wa nchi hiyo.
Mazungumzo hayo yamefanyika Machi 11, 2024 katika ofisi hizo kwa lengo la kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya Hakimiliki ikiwemo ukusanyaji na ugawaji wa mirabaha pamoja na sheria mbalimbali za Hakimiliki kwa kazi za ubunifu.
Amefanikiwa kujifunza namna nchi hiyo inavyokusanya mirabaha kwa kutumia Kampuni za Kukusanya na Kugawa Mirabaha (COLLECTIVE MANAGEMENT ORGANISATION -CMO'S) na kuzisimamia ambapo pia Tanzania inafanya jambo kama hilo kwa Wasanii na Wabunifu kupitia Kampuni ya TAMRISO inayokusanya mirabaha ya wanamuziki.
Kikao hicho kimefanyika kando ya mashindano ya Michezo ya Afrika (All African Games) yanayoendelea nchini humo ambapo Tanzania ni miongoni mwa nchi 54 zinazoshiriki michezo hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news