Tuwajibike sote kuwapa watoto wetu elimu sahihi kuhusu tatizo la dawa za kulevya!

DAR ES SALAAM- Ni wazi tatizo la matumizi ya dawa za kulevya limeendelea kutamalaki katika maeneo mbalimbali nchini.

Licha ya jitihada zinazofanywa na Serikali na taasisi nyingine zisizo za kiserikali kupambana na tatizo hili, bado matumizi ya biashara ya dawa za kulevya yameendelea kuwepo na kushika kasi huku wahanga wakubwa wakiwa ni vijana.

Hii ndio sababu Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za kulevya (DCEA) imeamua kuwekeza katika kutoa elimu ya dawa za kulevya kwa wanafunzi nchini. 

DCEA imekuwa ikizitembelea shule mbalimbali kufikisha elimu sahihi kuhusu tatizo la dawa za kulevya nchini, lakini ili kuweza kuwafikia watoto wengi ni jukumu la kila mzazi kumpa mtoto wake elimu hiyo ili aweze kutimiza malengo yake ya kusoma;

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news