PICHA:Rais Dkt.Samia akiwa na waliokuwa walinzi wa aliyekuwa Waziri Mkuu hayati Edward Moringe Sokoine

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na waliokuwa walinzi wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Hayati Edward Moringe Sokoine wakati wa Kumbukumbu ya miaka 40 tangu kifo chake, iliyofanyika Monduli mkoani Arusha tarehe 12 Aprili, 2024.
Kulia ni aliyekuwa Mlinzi Mkuu Abihudi Michael Luila aliyekuwa gari ya nyuma wakati ajali inatokea na kushoto Mlinzi wa zamu Yusto Chuma ambaye alikuwa gari moja na Hayati Sokoine. Chuma wakati huo naye alijeruhiwa vibaya sana na kulazwa chumba cha wagonjwa mahututi kwa siku 14.

Hayati Sokoine alifariki dunia tarehe 12 Aprili, 1984 kwenye ajali ya gari iliyotokea Wami Dakawa Wilayani Mvomero mkoani Morogoro.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news