Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Mei 11,2024

KATAVI- Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi imemchukulia hatua ya kumpumzisha majukumu yake, Mwalimu Ndikuliyo Mbatenga, anayedaiwa kuwalazimisha wanafunzi kuzibua vyoo vilivyoziba kwa kutumia mikono kama adhabu pasipo tahadhari yoyote ya kiafya.
Hatua hiyo inakuja baada ya wananchi wa Mtaa wa Kawalyowa Kata ya Ilembo kulalamikia kitendo cha Mwalimu huyo anayefundisha Shule ya Sekondari Kawalyowa kuwalazimisha baadhi ya wanafunzi kutoa kitu kilichosababisha choo kuziba kwa kutumia mikono.
Mwalimu Mbatenga anadaiwa kufanya kitendo hicho kama adhabu kwa wanafunzi hao aliodai walikula karanga wakati wanavuna katika shamba la shule.








Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news