Bosi wa Azania Group atunukiwa udaktari wa heshima kutoka Chuo Kikuu cha Harvard

WASHINGTON-Mtanzania,Ahmed Fuad Edha ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Azania Group ametunukiwa udaktari wa heshima wa ujasiriamali kutoka Chuo Kikuu cha Harvard nchini Marekani.
Edha anatakwa kuwa miongoni mwa wajasiriamali bora na wabunifu duniani.

“Tunampongeza kwa dhati Mkurugenzi Mtendaji wa Azania Group of Companies kwa kutunukiwa Udaktari wa Heshima wa Ujasiriamali kutoka Chuo Kikuu cha Harvard, taasisi maarufu duniani kwa ubora na ubunifu.

"Heshima hii ni ushuhuda wa uongozi wake wa kipekee, maono na mchango mkubwa katika kubadilisha maisha ya maelfu ya familia kupitia biashara na fursa Kusini mwa Bara la Afrika. Hongera sana kwa heshima hii muhimu,"imeeleza sehemu ya taarifa kutoka Chuo Kikuu cha Harvard.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news