Gavana Tutuba,Dkt.Kayandabila kushiriki mikutano ya msimu wa Kipupwe ya IMF na Benki ya Dunia

WASHINGTON D.C-Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba, pamoja na Naibu Gavana, Dkt. Yamungu Kayandabila, wanashiriki Mikutano ya Msimu wa Kipupwe ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na Benki ya Dunia inayoendelea jijini Washington D.C, Marekani.
Mikutano hiyo ya mwaka 2025 imebeba kaulimbiu isemayo “Ajira: Njia ya Mafanikio”, na inatarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 21 hadi 26 Aprili 2025.
Gavana Tutuba na Naibu Gavana Kayandabila ni miongoni mwa ujumbe wa Tanzania unaoongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb), ambaye pia ni Gavana wa Benki ya Dunia kwa upande wa Tanzania.Mikutano hii inatoa fursa kwa viongozi wa nchi wanachama wa IMF na Benki ya Dunia kujadili maendeleo ya kiuchumi duniani, changamoto zinazokabili mataifa mbalimbali, na fursa za ushirikiano wa kimataifa kwa ajili ya ustawi wa jamii.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news