Dkt.David Msuya ateuliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Fedha na Uchumi CCM

DAR-Mkuu wa Chuo Cha Mafunzo ya Ufundi Stadi cha Furahika kilichopo Buguruni Malapa jijini Dar es Salaam,Dkt.David Msuya ameteuliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Fedha na Uchumi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Buguruni.
Mjumbe wa Kamati ya Fedha na Uchumi CCM Kata ya Buguruni,Dkt.David Msuya.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa CCM Kata ya Buguruni,Saida A.Yamba uteuzi huo ulifanyika Machi 18,2025 katika kikao maalumu cha Kamati ya Siasa ya Halmashauri ya Kata.

Aidha,Dkt.Msuya baada ya uteuzi huo anatarajiwa kuhudhuria kikao cha pamoja cha Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya Kata kitakachofanyika Aprili 22,2025 katika ofisi za kata saa 10 jioni.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news