AfDB ni mdau muhimu kwa maendeleo ya Tanzania

ABIDJAN-Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb), kushoto, akifurahia jambo na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) anayemaliza muda wake, Dkt. Akwinumi Adesina, walipokuta katika Hoteli ya Sofitel Ivoire, Abidjan, Côte d’Ivoire, mahali ambapo unafanyika Mkutano Mkuu wa mwaka 2025, ambao utakuwa wa 60 wa Bodi ya Magavana wa AfDB na wa 51 kwa Mfuko wa Maendeleo wa Benki hiyo (ADF).

Mkutano huo ulianza Mei 26 hadi 30 Mei,2025, na utajumuisha uchaguzi wa Rais mpya wa Benki hiyo atakayemrithi Dkt. Adesina ambaye ni raia wa Nigeria na pia utafanyika uchaguzi wa Wakurugenzi Watendaji wa Taasisi hiyo kubwa ya fedha barani Afrika.
Zaidi ya wajumbe 6,000 wanatarajiwa kuhudhuria, wakiwemo Marais na Wakuu wa Serikali za Afrika, Mawaziri wa Fedha, Magavana wa Benki Kuu, washirika wa maendeleo, wawakilishi wa sekta binafsi, viongozi wa asasi za kiraia, wasomi, taasisi za utafiti, NGOs, na wadau wengine. Ukiwa na Kaulimbiu "Kufanya Rasilimali za Afrika Kufanya Kazi kwa Maendeleo ya Afrika".
Mhe. Dkt. Nchemba anamtaja Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB anayemaliza mhula wake, Dkt. Akwinumi Adesina, kuwa ni kiongozi mahiri na mtu muhimu katika maendeleo ya Tanzania tangu alipochukua uongozi wa Taasisi hiyo ambapo kupitia ufadhili wa miradi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii, Tanzania imepiga hatua kubwa kimaendeleo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news