DCEA yaongeza nguvu mapambano dhidi ya dawa za kulevya Mbeya

MBEYA-Katika harakati za kupunguza uhitaji wa dawa za kulevya nchini, Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa Kulevya (DCEA) imetoa elimu kwa viongozi wa serikali za mitaa 17.
Ni iliyotajwa kuwa na changamoto kubwa ya matumizi na biashara ya dawa za kulevya pamoja na viongozi wa asasi zinazotoa huduma kwa waraibu jijini Mbeya.

Mafunzo hayo yalilenga kuwajengea uelewa wa kina kuhusu tatizo la dawa za Kulevya, madhara ya dawa hizo na nafasi yao katika kutokomeza dawa za Kulevya kwenye maeneo yao.
Pamoja na elimu hiyo, viongozi hao walihimizwa kushirikiana kwa karibu na DCEA katika kutoa taarifa za matumizi na biashara ya dawa za kulevya kupitia namba 119 bila malipo.

Vilevile,kushiriki kikamilifu katika operesheni za kudhibiti dawa hizo na kutoa ushahidi mahakamani pale inapohitajika.
Hatua hii ni mwendelezo wa mkakati wa DCEA wa kuhamasisha jamii nzima kushiriki bega kwa bega katika vita dhidi ya dawa za kulevya.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news