Devotha Minja ajiuzulu uenyekiti CHADEMA,wajiondoa uanachama

MOROGORO-Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Kati, Devotha Mathew Minja ametangaza kujiuzulu nafasi zake zote ndani ya chama hicho na kujiondoa uanachama.
Uamuzi huo umeambatana na kujiuzulu kwa viongozi wengine tisa na wanachama zaidi ya 200 katika Manispaa ya Morogoro.

Minja amewaeleza wanahabari kuwa,hatua hiyo imefikiwa baada ya kutafakari kwa kina juu ya mustakabali wake kisiasa na kuona kuwa CHADEMA kimepoteza dira na lengo kuu la kisiasa ambalo ni kushika dola.

“Nimeamua kuondoka. Chama kimepoteza mwelekeo. Sasa ni wakati wa kutafuta mlango mwingine."

Kanda ya Kati inahusisha mikoa ya Morogoro, Dodoma na Singida ambako pia anatokea Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Tundu Lissu.

Minja ameeleza kuwa, kutoshiriki kwa chama hicho katika uchaguzi ni uamuzi wa watu wachache, ambao hauakisi nia ya wanachama walio tayari kupambana ili kushika dola.

“Msingi wa chama cha siasa ni kushika dola. Ukiacha kushiriki uchaguzi, hiyo dola utashikaje? Ndoto zetu za kuwatumikia wananchi haziwezi kufa kwa sababu ya misimamo ya watu wachache."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news