Kidato cha Sita kuanza mitihani kesho

DAR-Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limetangaza kuanza kwa mitihani ya kuhitimu kidato cha sita na Ualimu ngazi ya Cheti na Stashahada, inayotarajiwa kuanza kesho Mei 5, 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa NECTA Dkt. Said Mohamed amesema watahiniwa 134,390 wamesajiliwa kufanya mtihani wa kidato cha sita na watahiniwa waliosajiliwa kufanya mtihani wa ualimu ni 10,895.

Dkt.Mohamed ametoa wito kwa watahiniwa, wasimamizi, wakuu wa shule na wamiliki wa shule na vyuo nchini kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia mwongozo uliotolewa ili kuhakikisha mitihani hiyo inafanyika kama ilivyopangwa.

Ameongeza kuwa, NECTA tayari limekamilisha maandalizi yote ikiwa ni pamoja na kusambaza mitihani na nyaraka zote muhimu katika maeneo yote ili kufanikisha kufanyika kwa mitihani hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news