DAR-Mkuu wa Kitengo cha Sheria wa Yanga SC, Wakili Simon Patrick ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo kufuatia kushindwa kwa klabu hiyo kwenye kesi dhidi ya TFF, Bodi ya Ligi, na Simba SC katika Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo (CAS).
Kupitia mitandao ya kijamii, Patrick amesema anabaki kuwa mwanachama mtiifu wa Yanga huku akitangaza kupumzika na shughuli za soka.
“Vita dhidi ya wahuni haijawahi kuwa rahisi. Maamuzi ya CAS ni ya kuumiza, lakini viongozi wetu wamepinga uhuni kwa vitendo. Wana Yanga tuendelee kuwapa moyo,” amesema.