Rais Dkt.Mwinyi asisitiza malezi bora kwa watoto na vijana nchini

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dkt.Hussein Ali Mwinyi amezitaka familia kuweka dhamira ya kusimamia malezi ya vijana na watoto ili kuwa na Taifa lenye heshima na maadili.
Ametoa wito huo leo alipojumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika Sala ya Ijumaa Masjid Al Sahar Kwarara, Njia nne huko Wilaya ya Magharibi B.

Dkt.Mwinyi amesema, mambo mengi yanayojiri sasa ndani ya jamii yakiwemo ya wizi na uharibifu wa miundonbinu ya Serikali yanafanywa na vijana waliokosa malezi bora na Maadili ya Dini.
Amesema kuwa,mustakabali wa nchi yoyote unahitaji malezi ya vijana na watoto waliolelewa kwa maadili ili kuwa watu wema na wazalendo wa nchi yao.

Ameeleza kuwa, ni lazima kila mmoja kuwa na dhamira ya kusimamia malezi ya vijana ndani ya familia ili kuwa na watu wema watakaokuwa viongozi wa baadae.
Rais Dkt.Mwinyi amewakumbusha waumini hao umuhimu wa kuendelea kuiombea nchi amani hasa wakati huu ikielekea katika Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba,mwaka huu.

Amesitiza kuwa,bado Serikali inakusudia kutekeleza mambo mengi zaidi ya maendeleo katika nyanja tofauti,hivyo suala la kuwepo kwa amani ndio kipaumbele muhimu zaidi .

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news