Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Kigahe (Mb.), amekipongeza Chuo Kikuu Mzumbe kwa kuwatengenezea mazingira wanafunzi wa chuo hicho yanayohamasisha ubunifu, kujifunza mbinu za Ujasiriamali, uwekezaji na Biashara wakati wakiendelea na masomo yao chuoni hapo na hivyo kuwaandaa vyema kujiajiri na kutatua changamoto ya ajira na kuwawezesha kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa
Mhe. Kigahe ameyasema hayo wakati akimuwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selemani Jafo (Mb.), katika maadhimisho ya siku ya Chuo Kikuu Mzumbe na kambi ya Ujasiriamali iliyofanyika Mei 8,2025 Kampasi Kuu Morogoro na kuwataka wanafunzi hao kuitumia fursa hiyo vizuri kwa kufanya bunifu zinazoendana na kukua kwa teknolojia zitakazowezesha kutatua changamoto mbalimbali kwenye jamii na kuiwezesha Tanzania ya viwanda inayojitegemea kwa maarifa na teknolojia.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo