Vita dhidi ya dawa za kulevya ni yetu sote-DCEA

DAR-Katika kuendeleza ushirikiano wa kiutendaji kati ya Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) na Bodi ya Filamu Tanzania leo Ijumaa Mei 30,2025, Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo akiwa na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu, Dkt. Gervas Kasiga wametembelea Kikundi cha Jambo na Vijambo ambacho kinajihusisha na utoaji wa elimu ya kijamii kwa vijana hususani kuhusu madhara ya dawa za kulevya.Katika tukio hilo, Kamishna Jenerali Lyimo alieleza kufurahishwa kwake na kazi nzuri inayofanywa na Jambo na Vijambo katika kuelimisha jamii juu ya hatari za matumizi ya dawa za kulevya, huku akisisitiza kuwa juhudi kama hizo zina mchango mkubwa katika mapambano dhidi ya tatizo hilo sugu.
Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dkt. Gervas Kasiga, amemshukuru Kamishna Jenerali Lyimo kwa ushirikiano mkubwa anaoendelea kuutoa kwa tasnia ya filamu na michezo ya kuigiza katika juhudi za kupambana na dawa za kulevya.
Alibainisha kuwa ushirikiano kati ya DCEA na Bodi ya Filamu tayari umeanza kuzaa matunda, na kwamba wako tayari kuuimarisha zaidi ili kufanikisha mapambano haya kwa njia ya uelimishaji kupitia kazi za sanaa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news