NJOMBE-Wakulima wa parachichi mkoani Njombe wameishukuru Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia mbolea ya ruzuku ambayo imewasaidia kuongeza tija na uzalishaji katika zao hilo.

Mkulima mkubwa wa parachichi, Bw. Stephen Mlimbila, alieleza kuwa kupitia ruzuku hiyo, amepunguza gharama na fedha alizokuwa akizitumia kununua mbolea sasa zimeelekezwa kwenye ulipaji wa vibarua wanaohudumia shamba lake lenye ukubwa wa ekari 210 na kuwa chanzo cha ajira kwa wananchi wengi wasiokuwa na kazi.
Akijibu ombi la wakulima wa chama cha Ushirika Ng’anda cha kusajiliwa kuwa wakala wa mbolea za ruzuku, Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya TFRA, John Cheyo, amemwelekeza Meneja wa TFRA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bw. Joshua Ng’ondya, kuhakikisha Chama hicho kinasajiliwa na kusaidia kusambaza pembejeo hiyo kwa wanachama wake na kutatua changamoto ya ucheleweshaji pindi inapohitajika.
Cheyo alisisitiza kuwa serikali inatamani kuona wakulima wanaongeza tija na uzalishaji, akiwahimiza kulima kwa bidii ili kuzalisha mara mbili zaidi ya msimu uliopita ili kukuza uchumi wao.

Tags
Habari
Kilimo cha Parachichi
Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania
TFRA Tanzania
Wizara ya Kilimo Tanzania