ZANZIBAR-Young Africans Sports Club (Yanga SC) ya jijini Dar es Salaam imetwaa taji la saba la Michuano ya Kombe la Muungano.

Yanga ilitinga fainali ya michuano hiyo baada ya kuwatoa Zimamoto FC kwa mikwaju ya penalti 3-1, baada ya dakika 90 za nusu fainali yao kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Muungano Cup ni mahususi katika kuadhimisha miaka ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Muungano huo ambao ni zao la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwaka huu wa 2025 umefikisha miaka 61.
Kombe hili ambalo lilianza rasmi mwaka 1982 lengo ni kudumisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kutoa usawa wa kiuwakilishi katika michuano ya kimataifa ya vilabu.
Ni kutokana na Tanzania Bara kuwa na ligi yake na Zanzibar kuwa na ligi yake huku upande wa visiwani ukiwa sio mwanachama wa Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF).