CAIRO-Young Africans Sports Club (Yanga SC) imeangukia pua katika kesi yake ya awali iliyoifungua kwenye Mahakama ya Usuluhishi Michezoni (CAS).
Ni dhidi ya Shirikisho la soka Tanzania (TFF), Bodi ya Ligi (TPLB) na Simba Sports Club (Simba SC) ikiomba kupewa alama tatu na mabao tatu.
Vilevile iliitaka CAS izuie tarehe nyingine ya Kariakoo Derby isipangwe mpaka kesi ya msingi itakaposikilizwa ikiwa siku kadhaa zimepita tangu Simba SC kugoma kucheza.
Mchezo huo ulikuwa uchezwe Machi 8, 2025 hali iliyopelekea Yanga SC kupeleka kesi hiyo CAS wakigomea mechi hiyo kuchezwa tena.
Barua ya CAS iliyotolewa Mei 1, 2025 kwenye hukumu hiyo CAS imesema haina uhalali wa kisheria wa kusikiliza kesi hiyo yenye kumbukumbu CAS 2025/A/11298.
Ni kati ya Yanga SC, Simba SC, TFF na Bodi ya Ligi kabla halijapitia kwenye mamlaka za kisheria za TFF,hivyo imelifuta rasmi na kuliondoa shauri hilo kwenye mfumo wake wa mashauri.