KAGERA-Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeendelea na juhudi za kutoa elimu kwa umma kuhusu madhara ya dawa za kulevya kwa wananchi wa Wilaya ya Missenyi mkoani Kagera.
Elimu hiyo imetolewa katika maeneo mawili muhimu ikiwemo Soko la Bunazi na eneo la Mutukula lililoko mpakani mwa Tanzania na Uganda.Tukio hilo limeandaliwa kwa ushirikiano na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Missenyi, ambapo Katibu Tawala wa Wilaya,Bi. Mwanaid Mang’uro alimwakilisha Mkuu wa Wilaya na kuongoza shughuli hizo muhimu.
Aidha, baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya walihudhuria, jambo linaloonesha mshikamano wa pamoja katika mapambano dhidi ya matumizi na biashara ya dawa za kulevya.
Katika hamasa hiyo, wananchi walipewa elimu kuhusu athari za kiafya, kijamii na kiuchumi zitokanazo na matumizi ya dawa za kulevya.
Pia walihimizwa kushiriki kikamilifu katika kutoa taarifa pale wanapobaini vitendo vinavyohusiana na biashara au usambazaji wa dawa hizo haramu.
Tags
DCEA
DCEA Tanzania
Habari
Kataa Dawa za Kulevya na Timiza Ndoto Zako
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA)







