DCEA yafikisha elimu ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya kwa vijana waliokuwa kwenye mafunzo ya kijeshi

MTWARA-Afisa wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Pwani, Bi. Salome Mbonile ametoa elimu juu ya madhara ya dawa za kulevya kwa vijana wa Kampuni ya Ulinzi ya Assguard waliokuwa kwenye mafunzo ya kijeshi mkoani Mtwara.
Takribani washiriki 400 walifikiwa na kuelimishwa kuhusu athari za matumizi ya dawa za kulevya na umuhimu wa kutumia stadi za maisha waliyojifunza kwa njia chanya.

Aidha, walielezwa kuwa, matumizi ya dawa za kulevya yamezima ndoto za watu wengi, hivyo wana wajibu wa kushirikiana na jamii ikiwemo Serikali kupitia mamlaka katika kusaidia mapambano dhidi ya dawa za kulevya.
"Lakini yule mraibu anapokosa dawa za kulevya anapata arosto,akipata arosto anataka apate dawa za kulevya.

"Kwa hiyo, mraibu ni mtu ambaye hawezi kuishi bila kutumia dawa za kulevya, kwa hiyo ndugu yako akipata tatizo kama hili inaumiza sana,fikiria amefariki kwa sababu ya matumizi ya dawa za kulevya."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news