Lango la Likuyu na fursa endelevu sekta ya utalii na uchumi

RUVUMA-Katika bonde la kijani lililojaa mandhari ya kuvutia Kusini mwa Tanzania, Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma sasa inang’aa kama nyota mpya ya utalii.
Kupitia uwekezaji wa shilingi bilioni 2.1 kutoka Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, fedha hizo zimetumika kujenga miundombinu ya Hifadhi ya Taifa ya Nyerere ikiwemo lango la kisasa la kuingia Hifadhi ya Taifa ya Nyerereambalo limejengwa eneo la Likuyuseka Maganga na sasa, ndio mlango rasmi wa watalii kuingia hifadhi hiyo kupitia Nyanda za Juu Kusini.
Akizungumza kwa furaha hivi karibuni, Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Mhe. Ngollo Malenya, anasema ujenzi wa lango hilo umekamilika na sasa wilaya yake ipo tayari kuwakaribisha wageni kutoka kila pembe ya ukanda wa kusini,ikiwemo mikoa ya Lindi, Mtwara, Njombe, Iringa, Mbeya hadi Ruvuma, na hata nchi jirani kama Msumbiji na Malawi.
“Lango hili ni fursa ya kipekee kwa Namtumbo na Mkoa wa Ruvuma. Linakuza uchumi wetu kwa haraka na linafungua njia ya uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya utalii,” anasisitiza Malenya huku akitoa rai kwa wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza kwenye ujenzi wa hoteli, huduma za utalii na miundombinu mingine muhimu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news