Msihadaike na kelele za mitaani,twendeni tukaujaze uwanja Juni 15-Simba SC

DAR-Klabu ya Simba SC imesema ipo tayari kwa Derby ya Kariakoo kati yao na Yanga Sc itakayopigwa Juni 15,2025 huku ikiwataka mashabiki wakaujaze Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.
“Klabu ya Simba inatoa taarifa kwa Wanachama, Wapenzi, na Umma kuwa mchezo nambari 184 dhidi ya Yanga uliopangwa kufanyika tarehe 15/6/2025 upo kama ulivyopangwa.

"Tunawasihi msihadaike na kelele za mitaani, Wale ambao walinunua tiketi za mechi ya tarehe 8/3/2025 wazitunze kwa ajili ya matumizi ya mchezo huo na wale ambao hawajanunua tiketi wajiandae kununua baada ya tangazo la Bodi ya Ligi.

Twendeni tukaujaze Uwanja wa Mkapa.

"Inafahamika wazi kuwa Ligi Kuu ya NBC inajumuisha Timu 16 na si ligi ya timu moja, kwa mujibu wa taratibu kabla ya kuanza msimu,vilabu vyote 16 hushiriki vikao na kutoa mapendekezo ya kuboresha kanuni na taratibu ili kuimarisha ligi yetu,hivyo wenye hoja wafuate taratibu husika.

Tunaomba Bodi ya Ligi na TFF watoe hadharani ripoti ya uchunguzi juu ya wale wote waliohusika kuharibu mechi ya ligi jioni ya tarehe 7/3/2025 na wachukuliwe hatua stahiki na mamlaka husika.

Kutotolewa kwa ripoti na kutochukuliwa hatua kwa wanaoendelea kuchochea ghasia ni sawa na kulinda uharamia katika mpira ambao unatia dosari mafanikio yaliyopo katika tasnia ya mpira wa miguu nchini kwa sasa.”

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news