Uhamiaji yamzuia Godbless Lema kuondoka nchini

ARUSHA-Idara ya Uhamiaji imesema imemzuia Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA, Godbless Lema kutoka nchini na kuishikilia pasipoti yake katika kituo cha uhamiaji cha mpaka wa Namanga mkoani Arusha, pamoja na kumtaka kuripoti katika ofisi za Uhamiaji kwa ajili ya mahojiano.
Idara imesema kuzuiwa kwa Lema ni utaratibu wa kawaida unaotumika kwa raia yeyote pale ambapo idara imepata taarifa zinazohitaji mhusika kuhojiwa.

Aidha, imetoa wito kwa wananchi kupuuza taarifa zilizotolewa na Lema kupitia mitandao ya kijamii kuwa zuio hilo linawalenga viongozi wa CHADEMA.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news