Wananchi wamiminika banda la Wizara ya Fedha kupata elimu Maonesho ya Sabasaba

DAR-Wananchi wametakiwa kuhakikisha wanakopa katika maeneo rasmi ili kuondoa changamoto ya mikopo umiza ambayo imekuwa ikileta adha kwa wananchi kwa kufilisiwa mali zao.
Akizungumza katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara Dar Es salaam (Sabasaba) Afisa Mwandamizi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bi. Mary Mihigo amesema Serikali imeweka utaratibu wa kujisajili kwa watoa huduma za fedha ili kukomesha tatizo hilo.
Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara Dar Es salaam (Sabasaba) ambayo yameanza tarehe 28 Juni yanatarajiwa kuhitimishwa Julai 13 mwaka huu, ambapo Wizara ya Fedha na taasisi zake zinashiriki kikamilifu kutoa huduma kwa karibu kwa wananchi kupitia Maonesho hayo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news