Zimebaki siku sita kuelekea UMITASHUMTA na UMISSETA 2025 mkoani Iringa


MKOA wa Iringa unajiandaa kupokea wanamichezo kutoka mikoa mbalimbali nchini, katika Mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma Tanzania kwa shule za Msingi na Sekondari yanayotarajia kuanza tarehe 7 Juni 2025.
Mashindano hayo ambayo yanafanyika kila mwaka yanaratibiwa na Ofisi ya Rais-TAMISEMI ikishirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Kwa miaka mitatu mfululizo iliyopita tangu 2022, mashindano ya UMITASHUMTA & UMISSETA yalifanyika Mkoani Tabora, na mwaka huu yanafanyika Mkoani Iringa yakitarajiwa kuhusisha wanamichezo zaidi ya 7,000 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news