MAPUTO-Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Msumbiji ambaye pia anaziwakilisha Madagascar na Ufalme wa Eswatini, Mheshimiwa CP Hamad Khamis Hamad amekutana na Mhe. Antoine Kola Masala Ne Beby, Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) nchini Msumbiji kwenye Ofisi za Ubalozi huo jijini Maputo.
