Balozi CP Hamad ateta na Balozi wa DRC mjini Maputo

MAPUTO-Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Msumbiji ambaye pia anaziwakilisha Madagascar na Ufalme wa Eswatini, Mheshimiwa CP Hamad Khamis Hamad amekutana na Mhe. Antoine Kola Masala Ne Beby, Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) nchini Msumbiji kwenye Ofisi za Ubalozi huo jijini Maputo.
Wakati wa mkutano huo wa Julai 3,2025 ambao ni mwendelezo wa mikutano ya Mhe. Balozi Hamad kujitambulisha, waheshimiwa mabalozi hao walikubaliana kuendeleza ushirikiano wa kihistori kati ya Tanzania na DRC kwa maslahi ya pande zote mbili.
Katika hatua nyingine, Mhe. Balozi Beby ambaye ni Kiongozi wa Mabalozi wa Afrika nchini Msumbiji, alieleza kutambua na kushukuru mchango wa Tanzania kwa nchi yake katika maeneo mbalimbali hususan kwenye ulinzi na usalama.
Naye Mhe. Hamad aliahidi kufanya kazi kwa ukaribu na Mhe. Balozi Beby pamoja Mabalozi wengine wa Afrika waliopo Msumbiji ili kufanikisha Malengo ya Umoja wa Afrika.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news