Kikosi cha JWTZ kushiriki Gwaride la Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru wa Comoro

MORONI-Kikosi cha Wanajeshi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania kimewasili nchini Comoro ambapo kinatarajiwa kushiriki maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa nchi hiyo yatakayohudhuriwa pia na Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan atakayekuwa Mgeni Rasmi.
Kikosi hicho kikiongozwa na Captain Mohammed Maulid Nchimba kimetembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Comoro na kukutana na Balozi Saidi Yakubu pamoja na Mwambata Jeshi Kanali Abdulrahim Mahmoud Abdallah ambaye anaratibu ziara hiyo.
Akizungumza na askari hao Balozi Saidi Yakubu aliushukuru uongozi wa JWTZ hususan Mkuu wa Majeshi, Jenerali Jacob John Nkunda kwa kukubali mwaliko wa Jeshi la Comoro na kutuma kikosi chake kunogesha maadhimisho hayo. Mbali na Tanzania, wanajeshi toka China na Morocco nao pia watashiriki.
Balozi Yakubu pia alieleza kuwa, ushiriki wa JWTZ katika maadhimisho hayo ni kielelezo cha ushirikiano wa hali ya juu wa majeshi ya nchi hizo mbili na kuwaeleza kuwa mara zote vikosi vya JWTZ wamekuwa ni kivutio kikubwa wanaposhiriki na hivyo mwaka huu ni matarajio ya wacomoro kuws hali hiyo itaendelea na kuwaeleza pia makundi mengine yanayoshiriki toka Tanzania yallyoalikwa ikiwemo vikundi vya burudani na mabondia.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news