Benki Kuu ya Tanzania (BoT) yang'ara Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba)

DAR-Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imepata ushindi wa pili katika kundi la Taasisi za Udhibiti katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yaliyofungwa rasmi Julai 13, 2025, na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa (Mb).
Tuzo hiyo imetolewa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selemani Jafo na kupokelewa na Meneja Msaidizi kutoka Kurugenzi ya Usimamizi wa Sekta ya Fedha, Bw. Deogratias Mnyamani, kwa niaba ya Gavana Emmanuel Tutuba.
Ushindi huo ni uthibitisho wa jitihada thabiti na endelevu za Benki Kuu katika kuelimisha wananchi kuhusu majukumu yake pamoja na masuala mbalimbali yanayohusu huduma za fedha. 

Kupitia utoaji wa elimu hii, Benki Kuu inalenga kuwajengea wananchi uelewa wa kina kuhusu masuala ya uchumi na fedha ili waweze kushiriki kikamilifu katika mifumo rasmi ya kifedha na kufanya maamuzi sahihi yanayochangia ustawi wa mtu mmoja mmoja na maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news