Bima ya lazima kwa wageni wanaoingia nchini mbioni

NA GODFREY NNKO

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Sheria ya Bima Na.394 imeanzisha bima ya lazima kwa wageni wanaoingia Tanzania Bara itakayogharimu Dola za Marekani 44.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Julai 4,2025 na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kupitia Wizara ya Fedha,Bw.Benny Mwaipaja.

Kupitia bima hiyo, mchangiaji atanufaika na huduma za uokoaji, matibabu ya dharura, usaidizi akipoteza mzigo na kurudishwa nyumbani iwapo itatokea dharura.

Aidha,kupitia taarifa hiyo,Bw.Mwaipaja amefafanua kuwa, utekelezaji wake utaanza pale itakapoingizwa katika Gazeti la Serikali na umma utajulishwa;

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news