Gavana Tutuba aongoza Kikao cha 12 cha Kamati ya Uthabiti wa Sekta ya Fedha nchini

DAR-Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uthabiti wa Sekta ya Fedha Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba, ameongoza kikao cha 12 cha Kamati hiyo kilichofanyika tarehe 9 Julai, 2025 katika Ofisi ya Benki Kuu jijini Dar es Salaam.
Kikao hicho kinachohusisha mamlaka za Udhibiti na Usimamizi wa Sekta ya Fedha zipatazo 15 kimejadili masuala mbalimbali kuhusu Ripoti ya Uthabiti wa Sekta ya Fedha Tanzania ya Mwaka 2024.
Kamati hiyo inashughulika na masuala mbalimbali ya kustawisha sekta ya fedha yakiwemo kuimarisha usimamizi na kupunguza vihatarashi katika mfumo wa kifedha, mifumo ya usimamizi wa majanga katika sekta ya fedha, ushirikiano baina ya mamlaka za udhibiti wa sekta ya fedha na kuimarisha uwezo wa kifedha kwa watoa huduma za kifedha.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news