Gavana Tutuba atangaza Riba ya Benki Kuu (CBR) kwa robo ya tatu ya mwaka 2025

NA GODFREY NNKO

KAMATI ya Sera ya Fedha ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeamua kushusha Kiwango cha Riba ya Benki Kuu (CBR) katika robo ya tatu ya mwaka kwa asilimia 5.75 kutoka asilimia 6 iliyodumu kwa robo mbili za mwaka 2025,ikiwa ni mwelekeo wa riba itakayotumika katika soko la fedha baina ya mabenki.
Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw.Emmanuel Tutuba ameyabainisha hayo leo Julai 3,2025 makao makuu ndogo ya BoT jijini Dar es Salaam wakati akitangaza Riba ya Benki Kuu, baada ya kamati hiyo kukutana Julai 2,2025. Riba hiyo itatumika kuanzia Julai hadi Septemba,mwaka huu.

Hatua hii,pia ni kiashiria kimojawapo katika upangaji wa riba zinazotozwa na mabenki na taasisi nyingine za fedha nchini.

Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilianza kutekeleza mfumo huu Januari,2024 badala ya mfumo uliokuwa unatumia ujazi wa fedha.

Kupitia mfumo huu, Benki Kuu ya Tanzania huwa inatoa mwelekeo wa riba itakayotumika katika soko la fedha baina ya mabenki.

Lengo la Riba ya Benki Kuu ni kuwezesha ukwasi katika uchumi ili uendane na malengo ya kudhibiti mfumuko wa bei na kuwezesha ukuaji wa uchumi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news