GSM Group yasisitiza umuhimu wa afya njema kwa wananchi

DODOMA-Mkurugenzi wa Uwekezaji wa GSM Group, Eng. Hersi Said, amesema kuwa maendeleo ya taifa hayawezi kufikiwa bila afya njema ya wananchi na uwekezaji katika jamii.
Ametoa kauli hiyo wakati wa kilele cha NBC Dodoma Marathon 2025, ambapo GSM Group ilishiriki kama mdhamini mkuu kupitia taasisi yake ya kijamii ya GSM Foundation.

‎Katika marathon hiyo, GSM Group imetoa huduma kwa washiriki zaidi ya 12,000 kwa kuwagawia maji safi ya kunywa na vinywaji mbalimbali kutoka GSM Beverages ikiwemo G-Boost, GSM Pop na GSM Cola.
Kupitia GSM Foundation, kampuni imetoa msaada wa kijamii kwa kuunga mkono ajenda za marathon kama vile kuongeza idadi ya wakunga kutoka 100 hadi 200, kupambana na saratani ya mlango wa kizazi na kutoa ufadhili wa masomo kwa wauguzi 100 watakaohudumia watoto wenye changamoto ya usonji (autism).

‎Kampuni hiyo pia imewatunuku washindi wa mbio za kilomita 10 kwa wanaume na wanawake kwa zawadi mbalimbali zikiwemo vocha za bidhaa za kielektroniki kutoka Haier zenye thamani ya shilingi milioni 4, pamoja na vinywaji, sabuni na tambi kutoka GSM.
Kwa kutambua nafasi ya michezo katika maendeleo ya jamii, GSM Group imetoa wito kwa sekta binafsi na mashirika ya umma kuendelea kushirikiana kuwekeza katika afya na ustawi wa jamii kupitia matukio kama NBC Dodoma Marathon.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news