DAR-Klabu ya Yanga SC imetangaza kuachana na kiungo mkabaji, Khalid Aucho (31) raia wa Uganda baada ya mkataba wa kiungo huyo wa zamani wa Tusker FC, Gor Mahia za Kenya na Baroka Fc ya Afrika Kusini kufikia ukomo.
Aucho ambaye pia amewahi kuvichezea vilabu vya Red Star Bergrade ya Serbia, East Bengal na Churchill Brothers zote kutoka Ligi Kuu India alijiunga na Yanga SC mnamo Agosti 2021 na kuiongoza Yanga Sc kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu bara mara nne mfululizo.
Katika hatua nyingine, Aucho ameshukuru kwa huduma nzuri wakati akitumikia mkataba wake ndani ya Yanga SC;
