Magazeti leo Julai 1,2025

WAJUMBE wa Bodi ya Uongozi wa Wanajeshi Wastaafu (2024) SACCOS LTD na wadau wa maendeleo wamekutana kwa lengo la kuweka mikakati mbalimbali ikiwemo ya kutafuta ufumbuzi wa namna ya kusaidia Wanachama wa SACCOS ambao ni Wanajeshi wastaafu kuanzisha miradi ya uzalishaji mali.
Miradi hiyo inaweza kuanzishwa kwa kuanza na fursa zilizopo ndani ya mali asili ikiwemo aridhi,misitu,ufugaji nyuki ,samaki pamoja na fursa zingine za kimaendeleo zitakazoibuliwa katika mkutano huo wa bodi na wadau hao zote zikilenga kuinua,kuboresha, kustawisha maisha ya wanajeshi wastaafu kiuchumi na kijamii.


Akizungumza Juni 30,2025 jijini Dar es Salaam wakati akifungua mkutano huo maalum ambao pia uliwezesha washiriki kupokea taarifa ya robo mwaka, mgeni rasmi Meja Jenerali mstaafu Sharif Shehe Othman amesema kuwa,mkutano huo unaenda kutengeza historia mpya ndani ya SACCOS ya Wanajeshi wastaatu chini ya Sheria ya vyama vya Ushirika.


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news