Magazeti leo Julai 2,2025

Mageuzi makubwa ya sekta ya afya yamechochea mabadiliko ya maisha kwa maelfu ya wananchi wa Kagera baada ya hospitali, vituo vya afya na zahanati kusogezwa karibu na wananchi kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa hapo awali.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Hajjat Fatma Mwassa wakati akizungumza na waandishi wa habari Julai 1,2025 jijini Dodoma kuhusu Mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita kwa kipindi cha Novemba 2020 hadi April 2025 .

Mhe.Mwassa amesema,kati ya mwaka 2020 hadi Aprili 2025, Mkoa umefanikiwa kuongeza hospitali kutoka tatu hadi 11, vituo vya afya kutoka 29 hadi 42 na zahanati kutoka 217 hadi 283, hatua ambayo imepunguza umbali wa wananchi kufuata huduma na kuokoa maisha kwa wakati.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news